NYUMBANI
MAKTABA
_RelatedSite
KUHUSU SISI
WASILIANA NASI
_IyHAqoaspsitu
JINA
BARUA PEPE

_LATEST_BOOK
MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU UISLAMU
Hisn Al-Muslim
UISLAM NI
 
KATIKA IMANI ZA UISLAM
  • KATIKA IMANI ZA UISLAM:ni kuamini kuwa Ulimwengu pamoja na vilivyomo yupo ambaye ameviumba,naye ni Allah pekee hana mshirika,yupo juu ya mbingu(saba)anawaona na kuwasikia viumbe wake,naye ndiye pekee anayestahiki kuabudiwa na kuachwa ibada zote za asiyekuwa Allah.Pia katika sifa za uislamu ni kuamini ya kuwa Allah amewaumba watu ili wamuabudie na hakuwaumba kwa mchezo.Na siku ya kiama atawafufua na kuwahesabu juu ya matendo yao waliyoyafanya duniani.
 
KATIKA IMANI ZA UISLAM
  • KATIKA IMANI ZA UISLAM:Ni kuamini kuwa Allah anao malaika ambao amewaumba kwa nuru na akawapa kazi, hatuwaoni na wanatofautiana na wanadamu.kati ya hao ni Jibril ambaye amewakilishwa na Allah kufikisha wahyi(ufunuo)kwa Mitume.
 
KATIKA IMANI ZA UISLAM
  • KATIKA IMANI ZA UISLAM:Ni kuamini kuwa Allah ameteremsha vitabu kwa Mitume mfano:Taurati,Injili,Zaburi na cha mwisho ni Qur-ani ambacho kimeteremshwa kwa Mtume Muhammadi(s.a.w).Na vitabu vyote vilivyoteremka vinaamrisha kumuabudia Allah pekee bila ya kumshirikisha.Na vitabu vyote vilivyoteremka baada ya kupitiwa na muda mrefu maadui wa dini ambao wanakula mali za watu kwa batili waliingiza uharibifu mkubwa isipokuwa Qur-ani iliyoteremka kwa Mtume Muhammadi(s.a.wa)ndio pekee imesalimika kwa kiasi ambacho imehifadhika kikamilifu katika vifua vya watu,na huo ni muujiza aliyouweka Allah kwa viumbe pia Allah amedhamini kuihifadhi Qur-ani kwa kutopatikana mabadiliko na uharibifu,pia ni kitabu ambacho kinatawalia vitabu vyote vilivyotangulia.Na ndani ya Qur-ani kuna ushindi wa kisayansi ambao wasomi wa zama hizi wanathibitisha hilo.
 
KATIKA IMANI ZA UISLAM
  • KATIKA IMANI ZA UISLAM:Kuamini kuwa Allah amemuumba Nabii Adam kutokana na udongo na ni mtu wa kwanza kuumbwa,kisha akamfanyia watoto ili awape majaribio,baada ya muda mrefu kupita watu wakapotea na shetani akawapotosha wakaanza kuabudia masanamu,baada ya kutokea hayo Allah akapeleka Mitume wanaotokana na watu ili kufanya kazi ya kufikisha ujumbe ambao ni ibada ya kumuabudia Allah pekee bila ya kumshirikisha na kuwafuata Mitume na kuacha ibada ya asiyekuwa Allah.Miongoni mwa Mitume ni:(Nuhu,Ibrahim,Mussa,Isaa…)Na Muhammadi(s.a.w)ndiye Mtume wa mwisho.Na uislamu wa mtu yoyote hautokubalika mpaka aamini Mitume ya Allah na awapende.
 
KATIKA IMANI ZA UISLAM
  • -KATIKA IMANI ZA UISLAM:Ni kuamini kuwa kila kitu kinachotokea ulimwenguni ni katika makadirio ya Allah na tayari kimeshaandikwa kabla ya kutokea,pamoja na kuwa mwanadamu ameamrishwa kufanya mambo yatakayosababisha(utokeaji wa kitu hicho)na ndiye mfanyaji wa kitendo na anastahiki kuulizwa kutokana na mambo anayoyafanya na kila ambacho

    kitafatana na matendo yake duniani na akhera,na haifai kuacha kitendo kwa kutoa hoja ya makadirio.Itikadi hii itakufanya uishi kwa utulivu.
    6-Uislamu:Unaamrisha kufanya uadilifu,wema,kuunga undugu,kujizuia kutokana na machafu,ukweli…na sifa zote zilizo nzuri,na unakataza dhulma,zinaa,wizi,uadui kwa watu,kuua nafsi iliyohifadhika,uongo,kujifaharisha…na sifa zote zilizo mbaya,na baadhi ya makosa ambayo yanapatikana kwa baadhi ya watu ambayo hayalingani na uislamu hayo yote yanarudi kwa watendaji wa matendo hayo na uislamu uko mbali na makosa hayo.
KWANZA  1  2  3  4  5  6  MWISHO  

KURASA KUU
UISLAM NI
TOHARA
SALA
SALA TANO
Question And Answer
 
LUGHA
العربية Arabic
انجليزي english
صيني china
كينى Kenya
نيبالي nip
ألماني grmany
تجالوج TAGALOG
بيساو Bisaya
كلقان Kalagan
هندى hindi
تاميلي tamil
السواسيلندية Swaziland
بنقالية bangal
فيتنامي vitnam
هوسا Hausa
اليابانية Japan
تركي torke
روسي rose
اسباني Español
كوري cory
أندونيسيا indonesia
لينغالا-كونغو LINGALA
رواندا raounda
برمجة و تطوير الموقع اكساء لتكنولوجيا المعلومات